Jumatatu, Septemba 17

Umuhimu wa Massage kwa Wanamichezo (Benefits of Massage to Sportsmen)



Sports Massage ni aina ya massage inayolenga kuondoa mikazo ya misuli, maumivu na kuondoa sumu katika misuli ya wanamichezo ili waweze kuongeza ufanisi katika Michezo.

Ili mwanamichezo aweze kuongeza ufanisi ni lazima afanye massage kabla kwa ajili ya muiweka misuli yake imara ili iweze kumudu mikikimikiki ijayo. 

Ni muhimu pia baada ya michezo, mwanamichezo afanyiwe massage kwa ajili ya kuipumzisha misuli yake na kuondoa sumu(lactic acid) zilizojikusanya katika seli za misuli.

Jumanne, Mei 29

Maajabu Ya Kitunguu Swaumu

Ingawa watu wengi wanafahamu faida za vitunguu swaumu lakini bado wachache sana ndio wanaweza kupata faida zake ipasavyo.

Hii ni kwa sababu faida kubwa ya kitunguu swaumu inapatikana kupitia kampaundi yake ya sulphur hiitwayo Allicin ambayo hupatikana kwa kukisaga kitunguu swaumu kabisa.



Wengi humeza punje zake au kukikata katika vipande vidogovidogo na hivyo kukosa faida halisi ya kitunguu swaumu.

Vidonge vya Vitunguu Swaumu ni njia rahisi ya kuweza kupata faida halisi ya Kitunguu Swaumu katika mwili wako. Vidonge hivi vimebeba mafuta ya kitunguu swaumu yenye kampaundi ya Allicin ambayo hukupatia faida halisi ya kitunguu Swaumu.

FAIDA ZA KUTUMIA VIDONGE VYA VITUNGUU SWAUMU

1. Vinaboresha Mmeng'enyo wa chakula na kuondoa tatizo la gas tumboni.

2. Vinaboresha Afya ya Moyo kwa kuondoa lehemu ya ziada iliyoganda katika mishipa ya kupitisha damu.

3. Huboresha mfumo wa Kinga Mwilini. Huchochea ufanyaji kazi wa mfumo wa Kinga hivyo huupa mwili nguvu ya kupambana na magonjwa mbalimbali.

Vidonge hivi ni rahisi kwa matumizi na havikeri kwani
1. Havina ladha mbaya

2. Havitoa harufu kali kama inayotolewa na kitunguu swaumu chenyewe.

3. Ni rahisi kubebeka kwani vinahifadhiwa kwenye chupa.

Ili kupata Vidonge hivi wasiliana nasi kwa namba 0715343161

Happiness Massage

Jumanne, Aprili 24

BIG OFFER! Massage zote ni Tsh 50,000/= tu! Wahi sasa.

Kutokana na Maombi ya offer ya massage kuwa mengi sana. Na Happiness Massage dhima yetu (Our Mission)  ni kuboresha afya za watanzania, Tumetoa punguzo kubwa la bei ili kila mmoja apate fursa hii ya kuboresha afya yake kupitia huduma zetu nzuri za massage.



 Itumie Ofa hii sasa, Kuanzia jumanne hadi alhamisi.
 Massage yoyote unayopenda utapata kwa sh. 50,000 tu.
Tupo Lamada Hotel Ilala Dar es Salaam 

Simu : 0715343161.
 SMS: 0787 343 161
WhatsApp: 0756 343 161 / 0715 343 161
Happiness Massage-We bring back your happiness!

Jumapili, Machi 4

Athari za Maumivu Makali ya Mgongo na Suluhisho lake


Athari za Maumivu Makali ya Mgongo


Watu wengi huchukulia Tatizo La Maumivu Ya Mgongo kama jambo la kawaida na hawafahamu kuwa linaweza kupelekea matatizo makubwa katika mwili.
Tatizo la mgongo likiachwa kwa muda mrefu linaweza kupelekea:-

1.Ulemavu: Mtu anakuwa hana tena uwezo wa kusimama sawasawa na hivyo akitembea huelemea mbele. Hali hii humpa changamoto katika kuziendea shughuli za kila siku.

Jumamosi, Oktoba 7

Massage Tanzania


Massage Tanzania

Kama upo Tanzania na unahitaji Huduma Bora za massage, Karibu Happiness Massage Clinic 
Tunatoa huduma mbalimbali za massage, Tunakuhakikishia ubora wa Afya yako kupitia huduma zetu za massage, ushauri na virutubisho muhimu vyenye nguvu maradufu ya kulinda mwili dhidi ya Maradhi sugu na kuondoa sumu mwilini. 


Tunapatikana Lamada Hotel, Ilala Dar Es Salaam.
Fika ofisini kwetu kwa maelezo zaidi Au,
Tupigie 0715 343 161 au 0756 343 161

Ijumaa, Oktoba 6

Faida za massage ya Kichwa/ head massage

Massage ya Kichwa ina umuhimu mkubwa katika kuboesha afya ya binadamu, hasa ukuzingatia kuwa ni sehemu iliyobeba kiungo muhimu katika mfumo wa fahamu. Massage ya kichwa ikifanywa kitaalamu kwa kutumia mafuta maalumu ina faida zifuatazo:-
  1. Massage ya kichwa huboresha mzunguko wa damu kichwani, na kuwezesha damu nyingi iliyo safi(yenye oksijeni) kunawirisha afya ya ubongo na ukuaji mzuri wa nywele.

Alhamisi, Oktoba 5

Miguu/ Mikono kuwaka moto na ganzi ( Peripheral Neurapathy)




Tatizo la maumivu ya miguu au mikono na ganzi (Peripheral neuralpathy) hutokana na matatizo katika mfumo mdogo wa fahamu ambao huchukua taarifa kutoka sehemu mbalimbaili za mwili na kupeleka katika Ubongo kwa ajili ya kutafsiri na kutoa mwitikio stahiki. Tatizo hili husababisha Neva zilizo katika ncha za vidole hushindwa kupeleka taarifa hizo iusahihi, Kwa mfano zinaweza zikapeleka hisiia za maumivu hali ya kuwa hakuna kitu chochote kinachosababisha maumivu, Pia zinaweza zisipeleke taarifa za maumivu hata kama kuna kitu kinaumiza katika mguu au mkono-Hii ni hatari zaidi kwani mtu anaweza kuungua moto na asipate hisia zozote za maumivu.

Jumapili, Agosti 20

Massage inatibu Maumivu ya Kichwa


Tafiti zinaonyesha kuwa maumivu ya kichwa yanayosababishwa na msongo wa mawazo, uchovu au kukosa usingizi yanaweza kuondolewa kwa Massage.
Taasisi ya Marekani inayoshugulikia tiba ya Massage( AMTA= American Massage Therapy Association) imeongeza kuwa,  Pia massage:-
1.Inaondoa msongo wa mawazo.
2.Inapunguza hasira na.
3.Kurudisha mwili katika hali nzuri ya kiafya.

TUPIGIE Happiness Massage: 0715 343 161 _Kwa huduma bora za Massage_
Imeandaliwa na
-Happiness Massage-

Jumamosi, Agosti 12

Umuhimu wa Massage kwa binadamu na Dondoo muhimu.

Massage ni ukandaji na usuguaji wa sehemu ya mwili (ngozi, tishu, misuli) kwa kutumia mikono au mashine maalumu. Huduma hii hutolewa kwa lengo la:-
Kuondoa maumivu katika sehemu fulani ya mwili.
>Kulainisha misuli iliyokaza.
>Kuondoa uvimbe.
>Kuondoa uchovu wa mwili.
Kutibu jeraha.
>Kurelax.
>Kutibu saratani kwa kuondoa seli mfu.

Alhamisi, Julai 20

FAIDA 20 ZA MASSAGE KATIKA MWILI



1 Massage inaboresha afya ya ngozi.

2.Massage hufungua mishipa ya fahamu na kuongeza uwezo wa kufikiri.

3. Massage husafisha ngozi na kuboresha mfumo wa utoaji takamwili.

4. Massage inaondoa kovu la jeraha.

5. Massage husaidia kupona kwa wenye mivunjiko ya viungo au mifupa.

6. Massage huondoa uchovu wa mwili na kukosa usingizi.

7. Massage huzuia kansa ya ngozi na tishu.

8. Massage huzuia Saratani ya Matiti.

9. Massage huondoa maumivu ya wakati wa hedhi.

10. Massage huboresha mmeng'enyo wa chakula na kuzuia Constipation (choo kigumu au kukosa choo kwa muda mrefu).

11. Massage hupunguza maumivu ya uchungu kwa wamama wajawazito.

12. Massage huondoa uchovu na kuvimba kwa miguu kwa wamama wajawazito.

13. Massage huimarisha mifupa kwa kuchochea ufyonzwaji wa Madini ya Kalsiam(Calcium) na Fosforas.

14. Massage huboresha mzunguko wa damu mwilini.

15. Massage husaidia kuondoa maumivu ya misuli na majeraha.

16. Massage huchochea ufanyaji kazi wa homoni mwilini.

17. Massage huzuia Stroke/ kiharusi.

18. Massage inasaidia sana kwa wazee kuimarisha misuli na kuwapa nguvu ya kutembea.

19. Massage huondoa maumivu ya chini ya mgongo.

20. Massage husaidia kuboresha mfumo wa maji mwilini (lymphatic system) 

Tunapatikana Lamada Hotel, Ilala Dar Es Salaam.
0787 343 161
0756 343 161

Happiness Massage Tunaboresha Afya yako na kurejesha Furaha yako

Jumatano, Julai 19

Sababu za Maumivu Makali ya Mgongo



Kuna sababu  mbalimbali zinazoweza kupelekea maumivu ya mgongo nazo ni;
1.  Maambukizi katika pingili za uti wa mgongo: Maambukizi katika pingili za uti wa mgongo kama vile maambukizi ya saratani ya mifupa huweza kuleta maumivu makali ya mgongo.

2.  Kuvunjika kwa pingili za uti wa mgongo: Hali hiii inaweza kusababishwa na vitu mbalimbali hususani ajali ya kuanguka au kupinduka na gari.

3.  Umri mkubwa: Tatizo la maumivu ya mgongo mara kwa mara huwakuta watu wazima na wazee.

4.  Uzito kupita kiasi (Obesity): Uzito wa mwili kupita kiasi husababisha kuelemewa kwa uti wa mgongo na hivyo kuleta mgandamizo wa pingili za uti wa mgongo na kusababisha maumivu makali ya mgongo.

5.  Kukaa kwa muda mrefu: Kukaa kwa muda mrefu kama vile ofisini au madereva bila ya mazoezi hupelekea maumivu ya Mgongo.


6.   Mtindo Mbovu wa Maisha (Bad Lifestyles): Mtindo wa maisha kama vile kupuuza mbogamboga na vyakula vya asili hupelekea kuwa na mifupa hafifu na hivyo ni rahisi kuathirika hata kwa msuguo mdogo tu.

Jumatano, Septemba 21

TAHADHARI KWA WENYE MATATIZO YA PUMU(ASTHMA)

Pumu ni miongoni mwa magonjwa sugu ya hewa yanayosumbua  idadi kubwa ya watu Duniani hasahasa watoto.
   Tatizo hili limekuwa likiongezeka siku hadi siku,

Makala hii fupi inakusudia kutoa Tahadhari ambazo yapasa zichukuliwe kwa mwenye tatizo la pumu.


1.Epuka maeneo  yanayochochea shambulizi la pumu kwako kutokana na maelezo ya DAKTARI.

2.EPUKA VIPODOZI NA MANUKATO YENYE HARUFU KALI ambayo yanachochea pumu kwa upande wako.

3.Kula vyakulavyenye asili ya mboga za Majani kama vile nyanya, matango maharagwe mabichi, bilinganya na vyakula vingine vyenye asili hii.


4.MGONJWA ANAPASWA ATUMIE SAMAKI WABICHI KWA WINGI.


MAAJABU YA MASSAGE KATIKA MAGONJWA HATARISHI

.
Massage(Uchuaji)  ni tiba kongwe na ya uhakika katika kutibu magonjwa mbalimbali,kuanzia ya mwili na hata ya akili.Tiba hii ya massage huleta matokeo chanya pale itakapotolewa na Mtaalamu(Massage Therapist). Magonjwa mbalmbali tangu kale yamekuwa yakitibiwa na bado  hadi leo inaendelea kufanya kazi huku Wataalamu wakifanya tafiti mbalimbali ili kuzidi kuiboresha zaidi. Faida kubwa ya tba hii ni kwamba haina athari mbaya za kikemikali kwani dawa nyingi zinazotumika ni za asili (Organic).Miti mbalimbali hutumika katika kutengeneza mafuta yanayotumika kufanya massage.


Kuna magonjwa hatari ambayo yanaweza kutibika kupitia Massage. Hatari kubwa iliyopo ni kwamba watu wengi (hasa hapa Tanzania) huichukulia Massage kwa Mtazamo hasi na hii huwafanya wakose hata kufahamu kuwa massage ina umuhimu mkubwa katika Maisha yao.

Yafuatayo ni Magonjwa ambayo Massage imeonyesha Msaada Mkubwa katika kufanikisha kuyatibu. Na hii hutokana na Mbinu za kitaalamu zinazozifanywa  na watoaji wa huduma hii. Massage imeonyesha Msaada mkubwa katika kufanikisha kutibu Magonjwa yafuatayo.


1.MAGONJWA YA AKILI

Massage imeonyesha msaada mkubwa sana katika kutibu Magonjwa ya Akili.  Massage huamsha seli za ubongo na kuzifanya ziweze kufanya kazi katika hali iliyo nzuri. Hii ni kwa sababu magonjwa mengi ya akili tatizo huwa ni katika seli za ubongo ambazo hushindwa kupokea taarifa vilivyo kutoka katika Milango ya fahamu.

2.MAGONJWA YA KANSA

Kansa husababishwa na seli zisizo za kawaida katika mwili. Seli hizi zikiendelea kuwepo huziambukiza seli nyingine na hivyo kuongeza madhara zaidi. Suluhisho pekee ni kuziondoa seli hizo, Kwa sasa kuna Teknolojia ya kuziua Seli hizo zisizo za kawaida ili zisilete madhara zaidi. Massage ni njia bora kabisa ya kuharakisha kuziteketeza seli hizo. Hivyo kwa watu wenye Matatizo hayo ni vema wapate huduma ya massage itawasaidia.


3.MAGONJWA YA VIUNGO

Magonjwa mengi ya Viungo vya mwili yanatibika kiurahisi kupitia Massage. Uvimbe, kukaza kwa misuli, kukaza kwa viungo(joints) ni miongoni mwa Magonjwa yanayoweza kutibika kupitia massage.


4.KIHARUSI(STROKE)

Ugonjwa huu hutokea pale ambapo neva zinazosafirisha taarifa mwilini zinapokufa au kusimama kufanya kazi, Hali hii husababisha kukata kabisa kwa Mawasiliano kati ya Milango ya fahamu na Ubongo. Hivyo husababisha Mtu kushindwa kutumia hata viungo vyake kwa kuwa hakuna tena mawasiliano. Watu wengi wanapopata tatizo hili hukata tamaa kabisa na kuona kuwa huo ndio mwisho wa Maisha yao.Ukweli halisi ni kwamba , Massage imeonyesha ufanisi mkubwa katika kuharakisha Uponaji wa Tatizo hili. Kama mgonjwa atawahishwa. Kazi kubwa ya massage katika tatizo hili la kupooza ni kuamsha neva zilizolala ili ziendelee kufanya kazi kama kawaida. 

BEI ZETU NI SAWA NA BURE,
ILI KUPATA HUDUMA HII, FANYA BOOKING KWA KUPIGA SIMU

0715343161
0756343161
0787343161

instagram.com/happinessmassage

Jumatano, Septemba 7

MADHARA YA KUKAA KWA MUDA MREFU.

Habari na karibu mpenzi msomaji wa Happiness Massage Serrvices.
  Kama ilivyo ada ni wajibu wetu kukuelimisha wewe msomaji wetu.
Nianze kwa kutoa shukrani kubwa kwako wewe msomaji wa Blog hii.Tunathamini uwepo wako,Na Tunajitahidi kufany kila njia ili uendelee kupata maarifa mbalimbali.
   Afya ni kitu cha msingi sana katika m,aisha yetu,Hivyo ni lazima tujali Afya zetu ioli kuhakikisha tunaendelea kuwa bora kila siku na hivyo kufurahia Maisha yetu ya kila siku.

Jumanne, Septemba 6

UMUHIMU WA MASSAGE KWA WAZEE



Wazee wakiwa ni watu walio katika hatua ya Mwisho ya Ukuaji Wa Binaadamu huwa wanakutwa na matatizo mbalimbali.Hii inathibitisha kauli isemayo Uzee ni ugonjwa.


Bila kupoteza muda Mpenzi msomaji ningependa kwenda moja kwa moja kueleza Umuhimu wa Massage kwa Wazee kama ifuatavyo.
1.Massage huwapa nguvu wazee na hivyo wanaweza kutembea kirahisi.

2.Massage kwa Wazee huwaondolea hali ya kutetemeka kwa Viungo. Wazee walio wengi wana hali ya kutetemeka kwa viungo kitaalamu inafahamika kama Parkinson's disease. Massage ni tiba bora ya kumaliza tatizo hili.

3.Massage kwa wazee inasaidia kuongeza vilainishi vya viungo.

4.Massage kwa wazee huwasaidia kuondoa kukaza kwa misuli.

Alhamisi, Septemba 1

ITAMBUE THAMANI YA AFYA YAKO


Ni wajibu wetu kukuelimisha juu ya njia bora za kuboresha Afya yako ili iimarike na uweze kuishi kwa furaha, kumbuka afya ni uhai, pasipo afya njema hakuna raha tena ya kuishi. Kila kilichokuwa kwako kizuri na cha kufurahisha kinageuka na kuwa kibaya.

Kwa kulitambua hilo na kuthamini Afya Yako, Happiness Massage tumekusudia Kukusaidia.

Tunatoa huduma bora za Massage zinazolenga kuboresha afya yako na kurejesha Furaha yako ya asili.


 
0756 343 161
0715 343 161

KARIBU SANA HAPPINESS MASSAGE SERVICES.

Jumatatu, Agosti 29

UMUHIMU WA MASSAGE KWA WATOTO



Mtoto ni tunda bora linalotokana na Mti wa Ndoa. WanaNdoa walio wengi Duniani hujikuta katika furaha isiyo na kifani wanapopata Mtoto/Watoto. Wapo wanaosema kuwa Mtoto ni burudisho la Macho ya Wanandoa na hili si Uongo ni kweli kabisa. 

Mtoto  anahitaji apatiwe Huduma nyeti sana ambayo kutokana na huduma hiyo nyeti na muhimu ndiyo itakayomjengea msingi mzuri katika maisha yake yote atakayoishi hapa duniani. Huduma hiyo si nyingine bali ni malezi.  Na si malezi tu bali Ni malezi bora. Malezi yana maana kubwa sana kuanzia Kumpatia mtoto chakula bora, Mavazi, Huduma bora za afya na kuhakikisha kuwa Mtoto anakuwa na furaha, ni miongoni mwa vipengele vya Malezi. 

JE,WAJUA? 
Massage humuongezea Mtoto Furaha na si Hivyo tu, Bali pia Huboresha Afya ya Mtoto. Kama ulikuwa haufahamu basi kuanzia leo fahamu hivyo. Makala hii itajikita zaidi katika Kuzungumzia Umuhimu wa Massage Kwa Mtoto mdogo. Massage ina umuhimu mkubwa katika kuboresha Afya ya Mtoto na Kumuongezea Furaha. 

“Unapomfanyia Mtoto wako Massage,Bila shaka unausisimua Mfumo wa Fahamu”<Maneno haya Yalitamkwa na Dr.Tiffany Field kutoka Taasisi ya Uchunguzi ya Chuo Kikuu cha Miami (Marekani), Katika kitengo cha Shule ya Matibabu. 

Bila kwenda mbali zaidi Massage  humletea mtoto Mambo yafuatayo.

1.Humfanya mtoto apate Usingizi Mzuri. Hii ni kutokana na Masaage hulainisha viungo vyake na kumfanya mtoto awe katika hali nzuri ya kimwili.

2.Inaboresha Afya ya Mtoto. Kama ilivyotanguliwa kuandikwa kwamba Massage kwa mtoto husisimua mfumo wa fahamu. Msisimuko huo wa mfumo wa fahamu husababishwa kuzalishwa kwa Serotonin, ambayo ndiyo huleta furaha.Serotonin ndiyo pia inayosaidia kuongeza raha katika Tendo la Ndoa. Hii husaidia kupunguza mapigo ya moyo kwa mtoto na kumwacha mtoto akiwa na furaha muda wote.


Karibu Happiness Massage Tuboreshe Afya ya mtoto wako na kurejesha furaha yenu.

0715343161

Alhamisi, Agosti 25

JINSI MASSAGE INAVYOTIBU MSONGO WA MAWAZO



Msongo wa mawazo(stress) ni hali inayotokea kwa mtu baada ya kukumbana na tatizo fulani lisilokuwa zuri katika maisha yake. Hali hii humfanya mtu ajisikie mpweke,aliyeuzika na kukosa
furaha kabisa na hata kukosa hamu ya kula.Mara nyingi msongo wa mawazo hutokea kwa Vijana,lakini muda mwingine na kwa wazee pia.Msongo wa mawazo usipopatiwa
Ufumbuzi,hupelekea SIMANZI,ambayo ndiyo hali mbaya zaidi. Watu wengi hupata msongo wa mawazo lakini hawafahamu hali hiyo ndio msongo wa mawazo.Zifuatazo ni Dalili zinazoweza kuashiria msongo wa mawazo. 1.Maumivu ya kichwa 2.Uchovu 3.kukosa hamu ya kula 4.Kujihisi mpweke 5.kushindwa kufanya kazi zako za kawaida.  SABABU ZINAZOPELEKEA MSONGO WA MAWAZO Kuna sababu mbalilmbali zinazopelekea Msongo wa mawazo......
Sababu hutofautiana kutoka mtu mmoja na mwingine.Zifuatazo ni sababu zinazopelekea Msongo wa mawazo.
 1.Kufeli Mitiahani Mtu anapopata matokeo mabaya ya mitihani yake kinyume na alivyotarajia anaweza kupata msongo wa mawazo.
 2.Kuondokewa na mzazi/wazazi au mlezi/walezi au mtu wa karibu kama vile mwenza,ndugu, rafiki n.k huweza kumfanya mtu apate msongo wa mawazo.
 3.Usaliti katika Mapenzi Hii ni sababu kubwa kwa vijana inayopelekea msongo wa mawazo.Mtu aliyeasalitiwa huwa katika hali ngumu ya kihisia nahivyo kumfanya apate Msongo wa mawazo.Unapokosekana Ushauri kwa mtu wa namna hii huweza kumfanya achukue maamuzi mazito hata ya kujiua,na hii imeshuhudiwa mara nyingi sana ikitokea.
 4.Matatizo ya kifamilia Panapotokea matatizo ya kifamilia kama vile ugomvi au malumbano na usipofikiwa muafaka huweza kutokea msongo wa mawazo pia. Sababu nyingine zinazopelekea Msongo wa mawazo ni: Mikwaruzano na watu,Hofu ya tukio linalotarajiwa kama vile Mtihani,Kesi Mahakamani n.k. 

ATHARI ZINAZOTOKANA NA MSONGO WA MAWAZO 
1.KIFO Msongo wa mawazo huweza kupelekea kifo kama mhusika hatochukua hatua za kuiondoa hali hiyo au kama hatopatiwa suluhisho.Mfano mwaka 2013 kuna mwanafunzi aliyejiua kutokana na kupata matokeo asiyoyatarajia katika mtihani wake wa kidato cha nne.Hii bila shaka imetokea na msongo wa mawazo.

2.KUDORORA KWA SHUGHULI ZA KIUCHUMI KIUJUMLA. 
Kutokana na hali aliyokuwa nayo mtu mwenye msongo wa mawazo ni vigumu sana kufanya kazi na hata kama atafanya bado hakutokuwa na ufanisi.Hali hii hupelekea kushuka kwa shughuli za uzalishaji na hivyo huathiri hali ya uchumi.

3.MSONGO WA MAWAZO HUPELEKEA MAJONZI YA MUDA MREFU KWA MUHUSIKA. Kama msongo wa mawazo utaendelea kuwepo kwa muda mrefu bila kupatiwa suluhisho,inaweza kupelekea majonzi ya muda mrefu hali ambayo husababisha afya ya mhusika kuzorota. SULUHISHO LA MSONGO WA MAWAZO. Kabla sijaeleza kuhusu suluhisho la msongo wa mawazo,ningependa ufahamu kwanza.Kuna Njia tofauti zinazotumika kuondoa msongo wa mawazo.Njia hizi hutegmea ukubwa wa msongo wa mawazo. Kwa msongo wa mawazo wa kawida,njia zifuatazo zinaweza kumaliza kabisa tatizo hilo.

1.Massage ni Suluhisho bora kabisa katika  kuondoa Msongo wa mawazo. Kwa nini? Kwa sababu Wataalamu wa Massage(Uchuaji) wana ujuzi wa kutosha wa jinsi ya kushughulika na Mtu Mwenye Msongo wa mawazo kwa njia zote mbili(Kimwili na Kiakili). Na hii ndio tiba bora kwani mtu mwenye Msongo wa mawazo anaathirika kimwili(uchovu/kukosa nguvu) na kiakili.Wataalamu wanaotoa Huduma hizi za Massage(Uchuaji) kama vile Happiness Massage Services wanatumia Maarifa ya Fiziolojia na Saikolojia ili kuleta ufanisi katika tiba hii ya kuondoa Msongo wa Mawazo.Kitu cha kwanza kinachoathirika ni akili na baadae mwili hufuatia. Wataalamu wa Massage Hutumia mbinu muafaka ya kuanza kuondoa tatizo lililopo katika akili(ambalo huwa mawazo, huzuni, kujiisi mpweke, kufikiria mambo mabaya kama vile Kujiua) na baada ya kumweka mtu sawa kiakili Ndipo tiba ya Mwili inafuata.

Njia nyingine za kutatua tatizo hili la msongo wa mawazo n

2.Kutafuta mtu wa kuongea nae badala ya kukaa peke yako.

3.Kufanya mazoezi ya viungo.
Husaidia kuweka akili sawa na hivyo kurudi katika hali ya kawaida.

4.Kula mlo kamili. Mara nyingi mtu mwenye msongo wa mawazo hukosa hamu ya kula, na hali hii ya kukaa bila kula ndio huongeza zaidi tatizo, hivyo inashauriwa kujilazimisha kula. Ikiwa haya yote hayo yamefanyika na hakuna matokeo chanya, Msaada wa kitaalamu unahitajika kwa haraka kabla ya kuleta madhara zaidi.

Jumapili, Agosti 21

HISTORIA YA MASSAGE

HISTORIA YA MASSAGE Historia ya massage(uchuaji) inatokea mbali takribani miaka 5000 iliyopita miaka ambayo massage(uchuaji) ilikuwa ni njia kuu katika matibabu ya magonjwa mbalimbali.Si magonjwa ya viungo tu bali pia hata magonjwa mengine Michoro ya mapangoni inayopatikana sehemu mbalilmbali Duniani ni ishara/dalili tosha inayothibitisha kuwa tiba hii kongwe(ya massage) ilianza miaka